Рет қаралды 10,034
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amesema Daraja la JP MAGUFULI (Kigongo-Busisi), linalounganisha mkoa wa Mwanza na Geita, linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.
Akikagua Ujenzi wa Daraja hilo leo tarehe 24 Januari 2025 mkoani Mwanza, Waziri Ulega amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilion 611 kugharamia daraja hilo hadi sasa.