Рет қаралды 60,075
#CharlesWilliam #Zungu #Day2news
Majira ya saa moja usiku, tarehe 29 Oktoba mwaka 1948 Bi. Emelia Benezeti alijisikia uchungu na kujifungua mtoto wa kiume ambaye kwake na mumewe Petro Quamara alikua mtoto wa kwanza ambapo baadaye walifanikiwa kupata watoto wengine wawili, na kufanya familia yao iwe na na jumla ya watoto watatu wote wakiwa ni watoto wa kiume yaani Willibrod, Aloyce na Francis.
Katika hali ya kushangaza, siku ya kuzaliwa Willibrod, ambao wengi kwa sasa tunamuita Dk. Slaa, mama yake Bi. Emilia hakua akijisikia tofauti yoyote na alikua akiendelea na shughuli zake za kila siku. Ilipofika majira ya jioni mama huyo mjamzito alienda kuokota kuni vichakani na kisha aliporudi nyumbani alijisikia uchungu na kujifungua mtoto wa kiume, ambaye pia alipewa jina la “Slaa”, ikiwa ni sehemu ya kuelezea hatua ya mama kujifungua mara tu baada ya kurejea kutoka kuokota kuni.