Рет қаралды 26,248
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku ‘Msukuma’ jana leo alianza kufukua makaburi kuhusu basi lake lililokamatwa kwa kosa la kuwa na samaki watatu akisema linaozea kituoni lakini anashangaa aliyehusika yeye analalamika.
Msukuma ametoa kauli hiyo wakati akichangia katika hotuba ya makadilio ya mapato na matumizi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zilizochini yake ambapo amesema kuna watu huwa wanajisahaulisha wakisha kuwa nafasi za juu.
Hata hivyo Spika wa bunge Dk Tulia Akson amekea kauli hiyo akisema siyo sehemu ya mjadala ulio mbele ya bunge na kumtaka mbunge kujielekeza kwenye hoja mahususi huku akimsihi kufuta kauli yake aliyosema message delivery (ujumbe umefika).