Рет қаралды 4,000
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Alhaj Othman Masoud Othman, Leo Jumanne Agosti 13, 2024 amejumuika pamoja na Viongozi, Masheikh, Wananchi na Waumini mbali mbali wa Kiislamu, katika Maziko ya Marehemu, Bw. Sadra Hassan Juma, huko Wete- Mtemani, na Kangagani, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Marehemu Bw. Sadra, ambaye ni Mstaafu wa Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC), na pia Baba wa Mmoja wa Wasaidizi wa Mheshimiwa Othman, alifariki-dunia mapema Jana Agosti 12, huko katika Hospitali ya Mzena, Jijini Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu.
Marehemu amesaliwa katika Msikiti wa Ijumaa wa Mwitani Wete, katika Sala ambayo imeongozwa na Mjumbe wa Baraza la Ulamaa la Zanzibar, Sheikh Jamal Mohamed Abeid; kabla ya kupelekwa Kijijini kwao Kangagani, pia Mkoa wa Kaskazini Pemba, kwaajili ya Hatua za Mwisho za Maziko.
Viongozi mbali mbali wa Serikali, Siasa, Dini na Jamii wamehudhuria Maziko hayo wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Wete, Mhe. Dokta Hamad Omar Bakar na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Kichama Wete, Ndugu Juma Khamis Ali (kabakaba).
Awali kabla ya Maziko hayo, Mheshimiwa Othman amefika na kutoa, Mkono wa Pole kwa Ndugu na Jamaa huko Nyumbani kwa Marehemu, Kifumbikai Wilaya ya Wete, ambapo pia amewatakia Wanafamilia nyoyo za subra, hasa katika Kipindi hiki cha Msiba, huku akiwanasihi waendelee kuishi kwa umoja na mashirikiano, kama wakati ule ambao Mzee wao alipokuwa-hai.
Katika Tah-zia hiyo, Mheshimiwa Othman ameambatana na Mke wake, Mama Zainab Kombo Shaib.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi, Amiin!
Innalillahi Waina Ilayhi Raajiun!