Рет қаралды 16,870
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu ameshangaa baadhi ya wanachama wa CHADEMA na wanasiasa nje ya chama hiko wanaomkosoa kwa kitendo chake cha kutangaza hadharani kuwa kuna rushwa inaendelea kwenye uchaguzi wa ndani wa CHADEMA unaofanyika katika ngazi tofauti tofauti.
Akizungumza na wananchi wa Mpwapwa kwenye mkutano wa hadhara Lissu amesema kuwa haelewi wanaokosoa kitendo chake hiko wana lengo gani CHADEMA maana chama hiko kimekuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa kwa miaka mingi sana.