Рет қаралды 28,989
Safari ya kwanza ya treni ya umeme kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro imekuwa gumzo ikiondoka Dar es Salaam ikiwa limejaa abiria katika mabehewa yote.
Safari hiyo imeanza leo Ijumaa Juni 14 , 2024 wakiwemo Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC), Ally Karavina na Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Masanja Kadogosa.
Kama ilivyotangazwa, treni hiyo ilianza safari saa 12:01 asubuhi na inatarajiwa kutumia dakika 90 kufika Morogoro.
Mwananchi Digital itakuletea hatua kwa hatua za safari hiyo na kitakachojiri katika safari ya kwanza ya kihistoria ya treni hiyo.