Рет қаралды 61,456
Majibu ya Serikali Kuhusu Musiba, Diwani wa Zitto Aliyepotea!
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika, amefafanua leo Bungeni kwa kutoa majibu juu ya hoja mbalimbali zilizowasilishwa na wabunge zinazohusu idara yake, ikiwemo msimamo wa serikali juu ya matamko ya Mwanaharakati Cyprian Musiba na Kupotea kwa Mwenyekii wa Halmshauri ya Kibondo mkoani Kigoma.
Hoja kuhusu matamko yanayotolewa na Musiba iliwasilishwa Bungeni hapo na Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, ambapo Waziri Mkuchika, amesema idara ya Usalama wa Taifa inafanya kazi zake kwa siri, hivyo haitakaa itoe taarifa juu ya watu wanaowaita kuwahoji na kuwashughulikia.
Kuhusu Malalamiko ya kupotea kwa Mwenyekiti wa Halmshauri ya Kibondo, hoja ambayo iliwasilishwa na Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe, Waziri Mkuchika amesema serikali haipuuzii kupotea kwa watu nchini, isipokuwa suala hilo lipo chini ya jeshi la polisi na sio idara ya Usalama wa Taifa, hivyo watazidi kulisisitiza jeshi hilo kufanya uchunguzi wake kwa haraka zaidi na pia amempongeza Zitto kwa kumpigania Mwenyekiti huyo ambaye ni mwanachama wa CCM.
lnstal GlobalPublishersApp Android: bit.ly/2AAQe1d iOS: apple.co/2Assf4M Subscribe / uwazi FACEBOOK: / globalpublis. .
TWITTER: / globalhabari Visit globalpublishers.co.tz/, Subscribe / uwazi1
kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… / uwazi1 / uwazi1 / uwazi1 WEBSITE: globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: / globalpublis. . TWITTER: / globalhabari INSTAGRAM: / globalpubli .