Рет қаралды 14,074
Baba wa familia iliyotokea mauaji ya watu watatu katika Mtaa wa Segu Bwawani kata ya Nala, wilayani Dodoma Mjini, Robert Mugema ameomba Serikali kuimarisha ulinzi kwenye eneo hilo kwa kuwa wakati wa tukio kuna baadhi ya majirani nyumba zao zilifungwa milango kwa makufuli.
Septemba 16,2024 katika nyumba yake waliuawa watu watatu ambao ni Milcah Robert (12), aliyemaliza darasa la saba mwaka huu katika Shule ya Msingi ya Chilohoni pamoja na Mkazi wa Mailimbili jijini Dodoma Fatuma Mohamed (20) na kisha miili yao kuchomwa moto.
Katika tukio hilo pia binti aliyekuwa akifanya kazi katika nyumba hiyo, Makiwa Abdallah (16) aliuawa huku mama wa familia hiyo, Lusajo Mwasonge (40) akijeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
Akizungumza leo jioni Septemba 18,2024 nyumbani kwake Segu Bwawani mara baada ya ibada ya kuaga mwili wa binti yake Milcah, Mugemu amesema yeye atakwenda mkoani Geita kwa ajili ya mazishi ya aliyekuwa mfanyakazi wake wa ndani lakini familia yake itabaki kwenye nyumba hiyo.