Рет қаралды 1,083
Watu wawili wamepoteza maisha na wengine watatu wamenusurika kufa maji katika ziwa Singidani Mkoa wa Singida baada ya mtumbwi walioutumia kujaa maji.
Akielezea tukio hilo Simon Sambaa mwenyekiti wa mtaa wa bima kata ya Mitunduruni manispaa ya Singida eneo lililopo fukwe hizo amesema alipata taarifa kuwa vijana hao walifika eneo hilo kwa lengo la kutalii.
Sambaa amesema vijana hao walikodisha mtumbwi kwa ajili ya kuwapeleka kwenye jabali lililopo ndani ya maji kwa ajili ya kupiga picha ambapo kabla ya kufika mtumbwi ulijaa maji ambapo dereva alipiga mbizi na kujiokoa na wengine wawili waliokolewa na wavuvi huku wengine wawili walizama ambapo mpaka sasa miili yao haijapatikana.