Рет қаралды 886
Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania.
Mtangazaji na mwanamitandao Burton Mwambe alimaarufu kama Mwijaku ametakiwa kulipa faini ya tsh 5 bilioni kwa mtangazaji mwenzie Masoud Kipanya ni baada ya Mwijaku kuchapisha maneno ya kashfa dhini ya Masoud kipanya kwenye mitandao ya kijamii
hayo yamesemwa na wakili wa Masoud wakili Aloyce Komba leo Juni 15,2024 alipokua akizungumza na waandishi wa habari juu ya kesi hio ya mteja wake na Mwijaku na amesema kabla ya kuja mbele ya waandishi wa habari alimtaka Mwijaku kuomba radhi kwa njia ya maandishi kwao na kuita waandishi wa habari ili aweze kukanusha tuhuma ambazo alizotoa kupitia mitandao ya kijamii ila Mwijaku alikaidi na kufanya mkutano tu na waandishi bila kukiri kukosea kupitia njia ya maandishi na kufafanua ni aina gani ya biashara haramu alikua anazungumzia kuhusiana na mteja wake lakini hakufanya hivo amesema wakili huyo
ikumbukwe siku kadhaa zilizopita kupitia kurasa za mitandao za kijamii Burton Mwemba alichapisha maneno yenye jumbe za kumtaka Masoud Kipanya aweze kumuacha na maisha yake na kumtuhumu kwa kufanya bishara haramu