Рет қаралды 141
Imeelezwa kuwa Shahada ya Uzamivu ya Sayansi ya Misitu chini ya Mradi wa (REFOREST) inayotolewa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ni ya kipekee na itatoa wahitimu wabobevu katika sekta ya misitu na kusaidia kutunza na kulinda misitu hasa katika nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara .
Haya yamesemwa Juni 13, 2024 na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, na Uhaulishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Josephat Kashaigili wakati akifungua warsha ya uwasilishaji wa matokeo ya utafiti kwa wanafunzi wa Shahada ya Uzamivu kutoka SUA.
Prof. Kashaigili amesema wanasayansi hao wabobevu katika sekta ya misitu pamoja na kupata mafunzo lakini pia wamefanya utafiti katika nchi zao na kuwa mbinu hiyo ililenga kuimarisha ubora na kuongeza idadi ya wanasayansi wenye uwezo wa kufanya utafiti na kuwezesha wahitimu katika ukanda wa Jangwa la Sahara kuwa na ushirikiano katika uhifadhi wa misitu.