Рет қаралды 4,883
Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa ya matukio matatu ya watu kutekwa/kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kukutwa wakiwa wameuawa.
Tukio la kwanza ni tukio la Samwaja Sifael Said,miaka 22 mkazi wa Kijiji cha Chalunyangu kutoweka tangu Agosti 8,2024 katika mazingira ya kutatanisha na Agosti 23,2024 mwili wake kukutwa umefukiwa kwenye shimo huku sehemu zake za siri zikiwa zimekatwa.
Tukio la kutoweka kwake liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Makuro na lilifunguliwa jalada na uchunguzi kuanza.
Baada ya ufuatiliaji wa kina wa Polisi zilipatikana taarifa kwa kijana ambaye walikwenda kutizama mpira na Samwaja Sifael Said (marehemu) na baada ya mpira kumalizika walipokuwa wakirejea nyumbani walikutana na vijana wawili waliomwambia twende tukanywe pombe na walipoondoka pamoja hakurejea nyumbani na ndipo ndugu zake wakafika Polisi kutoa taarifa.
#sports #entertainment #BONGONEWSTV Usisahau ku-subscribe channel hii kwa taarifa nyingi zaidi na pia tembelea mitandao yetu ya kijamii Instagram @bongonewstz twitter @bongonewstz na Facebook @bongonewstz