Рет қаралды 1,593
Baba yake Chifu Mkwawa alijulikana kwa jina la Munyigumba Tengamahumba Chengamahomelo Muhomiyao Muyinga ambaye anasadikiwa kufariki miaka ya 1860 na kuzikwa katika kaburi lililopo Iringa kijiji cha Rungemba Halmashauri ya Mafinga wilayani Mufindi.
Baba yake Mkwawa alizikwa na mtu hai aliyefahamika kwa jina la Segeleni Mwang’owo aliyeingia kwenye kaburi na kumpakata marehemu na kuzikwa naye ambapo zamani ilikuwa ni fahari kuzikwa na Chifu hivyo watu wengi kugombea kuzikwa na Chifu.
Alipewa jina la Tengamahumba kwa sababu ya kuunganisha makabila kama vile Wahehe, Wazungwa, Wasagara na Wabena kuwa kitu kimoja.