Рет қаралды 27,052
Mtu mmoja ambaye ni Mwanajeshi, aitwae William Chacha Giriango (40) amekutwa amefariki kwa kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali yake aliokuwa ameutundika kwenye nondo ya dirisha katika chumba cha kulala Wageni kwenye Logde moja iliyopo Mtaa wa Hazina Jijini Dodoma.
Kamanda wa Polisi Dodoma, Martin Otieno amethibitisha tukio hilo ambalo lilitokea September 6, 2022 ambapo baada ya kupekuliwa marehemu alikutwa na meseji mbalimbali, ujumbe wa kwanza alimuandikia Mama yake ulisomeka “Mama yangu nisamehe sana nakuomba”
Kamanda Otieno amesema ujumbe wa pili alimuandikia Mke wake ulisomeka “kwako Mama Derick nisamehe sana kwa maamuzi haya, maisha kwangu hayana maana tena, nisamehe sana nimejitahidi nimeshindwa naomba uwatunze Watoto wetu"