Рет қаралды 841
NAIROBI. Kenya: HATMA ya Naibu wa Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua inajadiliwa leo kwenye Bunge la Kitaifa ili kupigiwa kura ima kusalia au kung’oka madarakani.
Iwapo thuluthi mbili (233) ya wabunge 349 itaunga mkono Gachagua kung’oka, hoja hiyo itawasilishwa kwa Seneti.
Hata hivyo ikiwa wabunge 117 wataikataa, Naibu wa Rais atasalia madarakani.
Bunge limekutana kwanza asubuhi leo kujadili hoja hiyo kama ilivyo kwa hoja nyingine yoyote kabla ya kumpa Naibu wa Rais fursa ya kujitetea, na baadaye kupiga kura kuthibitisha hoja 11 moja baada ya nyingine au kuzikataa zote.
Ikiwa mojawapo ya sababu hizo zitathibitishwa, hoja ya kumuondoa Gachagua itakuwa imepitishwa na spika ataliarifu Seneti kuhusu uamuzi wake ndani ya siku mbili
.
Bunge pia lina wajibu wa kumpa Gachagua haki ya kuchukua hatua za kiutawala za haki chini ya Kifungu cha 47 cha Katiba na haki ya kusikilizwa kwa njia ya haki kama ilivyoelezwa katika Kifungu cha 50 cha Katiba.
Video credit @ / @kenyacitizentv
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: ....
SpotiLeo: ....
TWITTER;
Twitter HabariLeo: Ha...