Рет қаралды 3,770
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linachunguza tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Edger Edison Mwakalebela (27), maarufu kama Sativa ambaye mkazi wa Dar es Salaam, Mbezi kwa Msuguri ambapo uchunguzi wa awali umebaini aliokotwa na wasamaria wema usiku wa kuamkia Juni 27, 2024 katika barabara ya Mpimbwe - Majimoto inayoelekea Mpanda katika pori la Hifadhi ya Taifa ya Katavi.