Рет қаралды 2,931
Wadau wamependekeza kufutwa kwa nafasi za ubunge wa viti maalum kwa kile kinachotajwa nafasi hizo zinachangia ukatili, hazileti dhana ya usawa wa kijinsia na kuigharimu Serikali zaidi ya Sh200 bilioni kila baada ya miaka mitano.
pendekezo hilo limetolewa leo Mei 25, 2024 katika ukumbi wa Hoteli ya Victoria Palace jijini Mwanza na Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Dk Ananilea Nkya, wakati wa mdahalo wa wazi wenye lengo la kujadili mchakato wa kupata Katiba Mpya ya Tanzania ulioitishwa na Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS).
Kwa mujibu wa Mchambuzi wa Masuala ya Kisiasa, Deus Kibamba, mwarobaini wa changamoto ya viti maalum bungeni itaondolewa kwa kuanzishwa kwa mchakato wa Katiba Mpya, mchakato alioutaja kwamba utaondoa mambo yaliyopitwa na wakati.
Hata hivyo alipopigiwa simu kuzungumzia maoni ya wadau kuhusu kufutwa kwa nafsi hizo, Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee amesema