Рет қаралды 13,902
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameielekeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, mara upelelezi utakapokamilika, kuwafikisha mahakamani mara moja watuhumiwa wote waliohusika na mauaji ya mtoto Asiimwe Novath aliyekuwa na umri wa miaka miwili na nusu mkoani Kagera, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaofikiria kufanya vitendo kama hivyo.
Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo bungeni jijini Dodoma leo asubuhi alipokuwa akiwasilisha tamko la Serikali kuhusu ulinzi wa mtoto ambapo amewataka wananchi kuachana na imani potofu au mizaha inayolenga kuaminisha kuwa viungo vya watu wenye Ualbino vinaweza kuwaletea utajiri.