Рет қаралды 22,529
Jumatatu ya Agosti 7 itakuwa ni juma moja limetimia la kutakiwa kuondoka madarakani kwa waliofanya mapinduzi nchini Niger.
Ni sharti lililotolewa na wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Uchumi ya Afrika Magharibi ECOWAS, vinginevyo nguvu ya kijeshi itatumika dhidi ya waliompindua rais Mohamed Bazoum.
Lakini pamoja na jumuiya ya kimataifa kutishia kuiwekea vikwazo Niger ili kushinikiza utawala wa kiraia kurejeshwa madarakani, msimamo wa rais wa sasa Jenerali Abdourahmane Tchiani aliyefanya mapinduzi ni kwamba mambo yao ya ndani yasiingiliwe.
Ni hoja iliyoungwa mkono na majirani zake nchi za Burkina Faso na Mali waliosema wapo tayari kumuongezea mwezao nguvu kuwaadhibu watakaoivamia Niger.
Karibu katika Chekeche