Рет қаралды 22,876
Post za kwenye mitandao ya kijamii pamoja na taarifa mbalimbali zilidai kuwa mfanyabiashara wa Zimbabwe Genius “Ginimbi” Kadungure, aliyefariki kwa ajali ya gari Jumapili ya November 8 mwaka huu, zilidai kuwa alinunua jeneza lake lililokuwa na gitaa jekundu juu wiki moja kabla ya kifo chake.
Ginimbi alifariki baada ya gari lake aina ya Rolls Royce kupata ajali na kulipuka baada ya kugonga mti na kuua watu wote wane waliokuwemo.
Hata hivyo, madai haya si ya ukweli, ni uongo mtupu, rafiki zake wamethibitisha kupitia shirika la habari la AFP, kwa kudai kuwa walinunua jeneza la brand ya Versace lililoonekana kwenye video wakati wanauchukua mwili wake kutoka ulikukuwa umehifadhiwa.