Рет қаралды 22,481
Alikuwa ulamaa mkubwa na msambazaji dini aliyefanikiwa kwao Zanzibar, lakini akaamuwa kuhamia Tanganyika kwa ajili ya kuendeleza kazi hiyo ya Muumba. Akatambuliwa, kuthaminiwa na kuaminiwa hadi akawa Mufti Mkuu wa Tanganyika nzima, akaungana na Watanganyika kuasisi na kukitetea chama cha ukombozi cha TANU kwa nguvu zake zote. Baada ya uhuru wa 1961, akafukuzwa kwa hizaya na kurejeshwa kwao Zanzibar, na kupigwa marufuku kuikanyaga tena ardhi ya Tanganyika kwa amri ya Mwalimu Julius Nyerere. Jina lake ni Mufti Hassan bin Ameir Al Shirazy.