TAREIKH YETU MSIMU WA KWANZA (SILSILA 10): Shujaa Abushiri aliyepambana na Waingereza na Wajarumani

  Рет қаралды 11,524

Gumzo la Ghassani

Gumzo la Ghassani

3 жыл бұрын

Jina lake hasa ni Salim bin Bashir bin Salim Al-Harthy. Umaarufu wake ni Abushiri. Alikuwa kijana, tajiri na shujaa. Alisimama dhidi ya Waingereza kwao Zanzibar. Akasimama dhidi ya Wajarumani kwenye ardhi ya Tanganyika. Zanzibar aliwaachia alama ya Jengo la Mambo Msiige. Tanganyika aliwaachia athari ya mapambano ya ukombozi. Mjuwe Shujaa Abushiri.

Пікірлер: 47
@kindysuleiman5935
@kindysuleiman5935 3 жыл бұрын
Mohammed unafanya kazi kubwa kutupa history ya kweli tuliyo hiniwa Allah akuwezeshe mwisho ukweli ubainike makatili wa kweli wabainike
@omarsaid673
@omarsaid673 3 жыл бұрын
Allah akuzidishie ufasaha na uwezo wa kutoa faida
@kindysuleiman5935
@kindysuleiman5935 3 жыл бұрын
Proud of you nitakosea nikisema wewe ni product ya Nabwa Allah amrehemu
@iddyramathan4507
@iddyramathan4507 2 жыл бұрын
Hongereni Sana Mohamed Ghassani kwa kutupatia historia halisi nilichojifunza watawala wa kiislam waliongoza watu wao vyema na walipendwa Sana na watu wao Ila walipoweka vibaraka Mambo yote yaliharibika.
@shaabanideauniversal6591
@shaabanideauniversal6591 3 жыл бұрын
Nimefurahi sana kusikia historia hii ya Al Bushir na Mambo msiige. Aidha ningependa pia siku moja tumzungumzie Bwana Muhmad bin Marjeb yaani almaarufu Tip tipp.
@khalifanassor9072
@khalifanassor9072 3 жыл бұрын
Subhanallah wazungu waliikamia zanzibar mpaka leo
@salumhamed5074
@salumhamed5074 7 ай бұрын
Historia mzuri sana
@fatmasaid5864
@fatmasaid5864 3 жыл бұрын
Uadui ulianza zamani
@khatibal-zinjibari6956
@khatibal-zinjibari6956 3 жыл бұрын
@Fatma Said. Maneno yako Sadaqta! Uadui ulianza zamani. Ninaomba kwa wasomaji samahani. Itakuwa ndefu kwani tumerithi uadui kwa Makafiri wanaoficha ukweli na kusambaza uongo wa Zanzibar na Oman kwa kuichukia dini ya Kiislam: "Wanataka (Makafiri) kuzima Nuru ya Mwenyezi Mungu (ya Uislam) kwa vinywa (Midia Propaganda) na Mwenyezi Mungu atakamilisha Nuru yake ijapokuwa Makafiri watachukiwa (Qur'an; 62:8). Mapotugizi ni Makafiri wa mwanzo kuanza Uadui kwa kuwauwa Waislam wa Zanzibar na Oman (1498-1700), Mapinduzi Matukufu kwa jina la Yesu. Baada ya Waislam wa Zanzibar kupigana na Makafiri kutoka Potugizi, Wafalme wa Zanzibar walikwenda Oman kuomba msaada kwa ndugu zao wa Kiislam ili kuwaondosha Makafiri wa Kikatoliki kutoka Potugizi. Ifahamike kwamba zama za Mtume Muhammad (pbuh) kadhalika Makafiri waliwaadhibu na kuwauwa Waislam wa Makka. Waislam walisaidiwa na ndugu zao wa Kiislam kutoka Madina baada ya Allah kusema: "Na mna nini (Waislam) hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu na (katika kuwaokoa wale Waislam) walio dhaifu katika wanaume na wanawake na watoto ambao husema: "Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalim na tujaalie tuwe (na) mlinzi anayetoka kwako na tujaalie tuwe na wa kutunusuru anayetoka kwako" (Qur'an; 4:75). Pengine kama si msaada wa Waislam kutoka Omani, Zanzibar isingekuwa kitovu cha Dini ya Kiislam na Kiswahili kwa Afrika Mashariki na Kati. Kadhalika akina Ali Hassan Mwinyi na Aboud Jumbe Mwinyi wasingekuja Zanzibar kusoma Uislam na Kiswahili. Labda kama si msaada wa Oman, Zanzibar igekuwa nchi ya Makatoliki kama Spain. Kabla Spain ilikuwa kitovu cha Uislam na Chuo cha mwanzo cha Timbuktu kilijengwa na Muislam wa Spain. Kabla ya Makafiri wa Kikatoliki kutoka Potugizi, Zanzibar ilikuwa maarufu sana hata mwandishi wa vitabu zaidi ya 100; Uthman bin Amar bin Bahr al-Furqayam al-Basr al-Jahiz (776-869) katika kitabu chake Al-Fakhar al-Sudan al-Abyadh (The Pride of Blacks Over to the Whites) amesifu mpaka wanawake wa Unguja na Pemba. Zanzibar pia ilitembelewa na Ibn Batuta kutoka Morocco. Wakati huo Zanzibar ilikua na sarafu zao kabla Christopher. Columbus kwenda (1492) Marekani. (G. S. P Freeman-Greenville (1957) Coinage in East Africa Before Portuguese Times. The Numismatic Chronicle and Journal of the Royal Numismatic Society Vol.17, pp.151-179). Ulimwengu mzima baada ya Morocco, Zanzibar ni Taifa la pili kuitambua nchi ya Amerika na kubadilishana mabalozi wakati wa Mfalme Said bin Sultan wa Zanzibar (1832-1856) na Rais Andrew Jackson (1829-1837) wa Marekani aliyemchagua Richard Palmer Waters (1828-1836) kuwa balozi alieandika: "They all welcome me to Zanzibar. I invited them to take a glass of wine with me, but they declined by saying that it was against their Islamic religion to drink wine." (March 18, 1837). Balozi huyo pia alidhamiria kusambaza Ukiristo Zanzibar kwa kuandika: "I have desired to be made to the Souls of these pagans among whom I am called to reside. That may going to dwell with may be a mean of introducing the gospel of Christ to them in that way may soon be opened for Missionaries to reside there. I desire to be made instrumental of good to that (Zanzibar) people. May the Lord increase the desire." (January 1, 1837). Balozi Richard Wateres alihubiri Gospel kwa Sultani Said mpaka hadharani na aliandia: "I often talk with them (Zanzibar Muslims) on the interest of the Soul and they most always reply by saying: "Our book (Qur'an) speaks all the same as yours and we pray plenty." (January 1, 1837). Wakati wa utawala wa Kiislam Zanzibar, Mkirsto wa Marekani alihubiri Gospel hadhari kwa sababu Allah anasema: "Hakuna kulazimishana (mtu kuingia) katika dini. (Qur'an; 2:256). Baada ya Muungano, Mashekhe wa Zanzibar waliohubiri nchini kwako kutaka Uhuru bado wako jela ya Tanganyika. Sayyid Said bin Sultan alimteuwa Nahodha mahiri na gwiji wa Kiswahili, Kiingereza, Kiarabu na Kifursi Al-Hajj Ahmed bin Nouman bin Muhsin (1784-1870) kuwa Balozi wake wa Marekani. Meli ya SULTANA ya Sayyid Said alitua nanga New York na ya mwanzo kutoka Afrika kwenda Marekani. Makamo wa Raisi wa Marekani Richard Mentor Jackson (1837-1841) aliitembelea Mali ya SULTANA na Raisi wake Martin van Buren (1837-1841) alimwandikia Sayyid Said bin Sultan: "It was a source of lively satisfaction for me, in my desire that frequent and beneficial intercourse should be established between our respective countries (Zanzibar and America) to behold a vessel bearing your Highness's (Zanzibar) flag enter a port of the United States." (Jeremy Prestholdt. The SULTANA in New York: A Zanzibaibari Vessel Between Two Worlds). Leo bendera ya Zanzibar haijulikani nje ya Zanzibar wakati ilikuwa maarufu Afrika nzima baada ya Egypt na kabla ya Muungano, Zanzibar ilikuwa tajiri kuliko nchi zote za Afrika Mashariki kutokana karafuu aliyoleta Mwarabu na Sayyid Said bin Sultan akaisambaza Unguja na Pemba. Lakini siasa imefanya bei ya karafuu kudidimia na utalii unaoleta malaya na madawa kushika bendera 😂😂😂 Said Majid bin Sultan (1856-1870) alijenga eneo na kuita Dar as Salaam, ambalo limetamkwa kwenye Qur'an. Maadui wa Kiislam kwa kisingizio cha Uarabu, Dar as Salaam wameliita Bandari Salam. Wengine walisema lipewe jina la asili la Mzizima. Kama ni hivyo, jina la asili ya Tanzania ni Tanganyika. Baada ya Muungano, majina ya Dar as Salaam na Zanzibar hayatakiwi. Badala yake Dar as Salaam iitwe Mizizima na Zanzibar iitwe Tanzania Visiwani. Waliotaka Zanzibar kwa Wazanzibari kama vile Muhammed Salim (Jinja), Abeid Amani Karume na Ameir Soud wa Bwejuu, wameuliwa kinyama. 😅😅 Tofauti na wanaotaka Kenya kwa Wakenya au Tanganyika kwa Watanganyika kama Rev. Christopher Mtikila na kundi lake la G55 waliotaka Serikali ya Tanganika. Hawambiwi wataleta Wajarumani au Waingereza kwa sababu wa ni Wakiristo!!
@fatmasaid5864
@fatmasaid5864 3 жыл бұрын
@@khatibal-zinjibari6956Mashallah shukran inaonesha historia unaijua vizuri Jazakah Allah kheir akhi al azizi
@msabahaali758
@msabahaali758 2 жыл бұрын
Alla amrehem shekhe Abushir ukijitoa kwa ukweli kutetea ardhi za Waafrika
@zeanamohamed4072
@zeanamohamed4072 3 жыл бұрын
Hii historiya inasikitisha kumbe Zanzibar imianza kuhuyumiwa Zama waliyonyongwaa mungu awalaze mahala pema peponi aminni
@salumhamed5074
@salumhamed5074 7 ай бұрын
Safi sana
@imraniqbal00765
@imraniqbal00765 3 жыл бұрын
Assalam aleiykum Shukran sanaa kwa kutujuvya haya
@GumzolaGhassani
@GumzolaGhassani 3 жыл бұрын
KHAMIS khamis Alaykum salam warahmatullah. Afwan
@sulaly1
@sulaly1 3 жыл бұрын
Masha Allah kitu kimegonga kwenye ubongo
@salumhamed5074
@salumhamed5074 7 ай бұрын
Nice
@salumhamed5074
@salumhamed5074 7 ай бұрын
ممتاز
@saidhamad7504
@saidhamad7504 3 жыл бұрын
Kaka Mohd hali zenu.. tnasubr kwa mda kpata vpnd vipya.. tnatumai mtatuandalia vpndi vpya kila siku
@mohammedbinjumaabinaweisal9188
@mohammedbinjumaabinaweisal9188 3 жыл бұрын
Kwa Hakika vijana tunanyishwa sumu, Na kusaulishwa utu,na hadhi na heshima yetu Mungu awarehemu waliotangulia akhera.
@salumhamed5074
@salumhamed5074 7 ай бұрын
Good
@hashilfarahani4024
@hashilfarahani4024 3 жыл бұрын
Assalamualaykum warahmatullah wabarakatuh?,Kwanza hongereni sana sana kwa kutoa elimu ya kihistoria Allah awazidishie mema,Pili samahani naomba kujua Mzee kipindi hicho ulikua kama nani au ulisoma tu kama tunavyosoma sisi?.
@rukiamohammed9451
@rukiamohammed9451 3 жыл бұрын
SUBHANA LLAH
@fatmasaid5864
@fatmasaid5864 3 жыл бұрын
Historia ya Zanzibar yote ni ya kusikitisha
@alhabsi6430
@alhabsi6430 2 жыл бұрын
Kweli kabisa
@omarsaid673
@omarsaid673 3 жыл бұрын
Nahusudu kiswahili cha Nd yangu Ghassani.
@basharahamtzhalisi6871
@basharahamtzhalisi6871 3 жыл бұрын
Hahaha! Hata mimi ndugu yangu, WALLAH anazungumza kwa mvuto uliopangika wa kilugha ktk ulimi.
@meyou-zz8mj
@meyou-zz8mj 3 жыл бұрын
Salaam alyeikum....tufungulie mafile ya kilwa kivinje na story ya sarafu yake
@iddyramathan4507
@iddyramathan4507 2 жыл бұрын
Kumbe majinga ya usaliti mapenda kula haijaanza leo
@AM-xi4sy
@AM-xi4sy 3 жыл бұрын
huyoo ni omar Muktat
@neronapoleon6054
@neronapoleon6054 Жыл бұрын
Abushiri hakuwa mzalendo , alikuwa mfanyabiashara wa utumwa alituuza wazingua kama anauza karanga
@eastafricaqualitychickenfa9916
@eastafricaqualitychickenfa9916 21 күн бұрын
Muongo so nyamaza tu kama hujuwi
@adamalbalushi1009
@adamalbalushi1009 3 жыл бұрын
Correction; Riadh Al-Busaidi aliposema jina la Chief "Kawawa", jina lake lilikuwa Chief Mkwawa, Chief wa kabila la wahehe. Alipigana na wajerumani kwenye vita iliyojulikana kwa jina la vita ya MAJI MAJI. Jazakum ALLAHU Khairan Mohammed, hii ndiyo real history sio ile iliyoandikwa na wacolony.
@4pesa
@4pesa 3 жыл бұрын
Ma boati kubwa zina it was jahazi
@bakariahmadi9645
@bakariahmadi9645 3 жыл бұрын
Huyu mjerumani nimtu m baya anatakiwa alipe fidya kwa aliyo ya fanya
@111dudi
@111dudi 3 жыл бұрын
Viongozi wa Znz wanaotutuhumu waarabu kwa kufanya biashara ya utumwa, waangalie hii clip wamjue huyu mwarabu muomani aliyechanganya na mwafrika ambae alikufa kwa huihami Afrika. Na wakome kusema maneno ya utumwa na uchotara. Wajue maadui wa waafrika ni wazungu hasa waingereza na wajerumani
@salehally8007
@salehally8007 3 жыл бұрын
Yanahusiana na nn hayo tena naona una ropokwa tu hujui ulisemalo una lako jambo
@Nedjadist
@Nedjadist 3 жыл бұрын
Sasa wataka kupinga hakukuwa na biashara ya utumwa? Na kama ilikuwapo nani aliifanya? Na ilimalizikaje? Haiwezekani mtu aliyekuwa anamwuza mwingine, siku moja aamue tu kuwa 'yatosha'. Tofauti ya nyie Waarabu na Wazungu ni kuwa Mzungu at least anakiri mabaya aliyoyafanya. Ama nyie, hadi leo hamjali machungu aliyoyapata Mwafrika. Mmeitia aibu kubwa dini ya Kiislamu nyie Mapagani wa Kiarabu, hadi ikawa synonymous na Utumwa! Mkahalalisha unyama wa kuteka watu na familia zao kutoka kwenye majumba yao, kisa ni weusi. Katika Uislamu mtumwa ni 'yule tu aliyekamatwa katika vita vya kutetea Uislamu' Sasa hawa watumwa kwa mamilioni mliowauzia Wazungu, na wengine mkawakhasi na kuwapelekea Arabuni, dini gani inasema hilo ni halali? Na hata huko Arabia, jinsi mlivyowatesa kwa unyama wenu mpaka wakafanya maasi Basra, kusini ya Iraq, yailiyojulikana kama 'Maasi ya watu weusi' mwaka 869-883. Pande zote mbili, Wazungu na Waarabu, huongeza chumvi wanapozungumzia unyama wa upande mwingine, lakini ukweli utabaki vile vile kuwa wote wawili na wataendelea kuwa maadui wa Mwafrika. Vita vyao kimsingi vilikuwa kumzuia mmoja asile, wala siyo kumtetea Mwafrika. At least, Mzungu anamwona Mwafrika 'hajastaarabika', ama Mwarabu humwona ni 'mnyama tu' ambaye unaweza kumchinja, kumfuga, au kumwuza! Kuendelea kutetea unyama huo inamaanisha kwamba hata hii leo kusingekuwa na sheria zilizoletwa na Mzungu mngekuwa bado mnaendelea kutuuza. Usinikasirishe nikakutukana, maana historia iko wazi na wala huna haja ya kuchochewa na mtu, nenda Zanzibar, Kilwa nk utaona mahandaki waliochimbiwa watumwa. Baadhi yetu babu zetu hasa wametusimulia personal experiences za unyama wa Mwarabu. Kwenda zako. By the way, mimi ni Muislamu, ila si Uislamu wako wewe na Mapagani wengine wa Kiarabu!
@111dudi
@111dudi 3 жыл бұрын
@@Nedjadist Biashara ya utumwa ilikuwepo, na ilifanywa na waafrika wenyewe, wazungu, wahindi, wafurs, wahindi,waarabu etc, sio kuwasakama waarabu peke yao. Kuna waarabu znz walikuwa wanawanunua watumwa ilikuwaacha huru, hawa hawazungumzwi hata siku moja. Mmekalia kuwasema waarabu ,waarabu na mnasahau kuwa taifa likichanganya dam na waafrika kuliko mataifa yote ni waarabu. Hebu chunguza kuna machotara wangapi wa kizungu au kihindi? Fungueni macho.
@Nedjadist
@Nedjadist 3 жыл бұрын
@@111dudi Huwa nashangaa sana kwa nini Waarabu kwa ujumla hawapendi ku 'own up" to their dark past. Ukiwaambia ndiyo husema hivi, kuwa hata wengine walifanya! Hata wengine walifanya kwa hiyo nyie mkafanya pia? Lakini nyie si mna dini? Halafu si kweli hiyo 'hata wengine walifanya" Walivyowafanyia Waafrika, hakuna mwingine amefanya. Yaani mtu kuja na bunduki na jeshi lake, kukisakama kijiji kizima, kuchoma moto nyumba zote, kuwakusanya mama, baba, watoto...kuwauwa au kuwamaliza wale wasiojiweza na kuanza safari ndefy, ngumu, ya machozi na wengine zaidi kufa njiani kuelekea sokoni...... Niambie nani amefanya hivi? Utumwa wa Mwafrika kwa Mwafrika ulikuwa wa watu waliokamatwa vitani (at least wana aina ya makosa) au walioasi taratibu za kabila. Hawa hutelekezwa na kuuzwa kwa kabila jingine. Ingawaje lengo hapa si kujipati manufaa ya kifedha ili wajenge Makasri na waowe wake zaidi.... C'mon! How do you compare the two? One is selling you like a goat, treatign you like a goat and one just wants to get rid of you because you are a POW or a nuisance.... Halafu uone kwamba hili lilifanywa kwa dhamira ya ubaguzi zaidi...Waarabu pia waliwafanya watumwa watu wengine weupe, kama Sharkas, lakini hao hawakuwaita watumwa "abd' waliwaita 'Mawali' na jinsi walivyokaa nao ni tofauti kabisa na watu weusi. Hakuna katika "mawali' aliyekatwa pumbu kwa mfano. Bahati yenu watu weusi ni watu wa kusamehe sana na kusahau. Imagine ingekuwa mmewafanyia hivi Warumi au Wayahudi......
@111dudi
@111dudi 3 жыл бұрын
Kumbe wewe unaonekana umesoma historia ya wazungu, waliokuja na biblia nkono mmoja na bunduki mkono mwingine. Fatilia KZbin Gumzo la Ghasani upate uhakika. Hao wakina Longstone na majasusi kama yeye walitumwa Afrika kuja kufitinisha baina ya waafrika na waarabu kwa akujifanya wao ni watu wema. Soma malengo ya mkutano wa Berlin ujue uadui wao. Waarabu na waafrika waliishi kwa amani mpaka walipokuja wazungu. Wafanya biashara ya utumwa wazungu walitumwa na Malkia wa Uingereza, kuja Afrika kuchukua watumwa. Unajua Livingstone alimkana mtoto aliyezaa na mkongo? Na akamterekeza? Hebu semeni historia iliyoandikwa na wasio wazungu mpate ukweli na muache kutusakama . Lugha, mavazi, dini, ustaarabu tumewaletea, hamshukuru hivi? Mkekalia waarabu na utumwa, waarabu na utumwa. Hhee. Huyo Livingstone mwisho aliandika kuwa alidhania tuu kama waarabu walifanya biashara ya utumwa hakua na uhakika.
@iddyramathan4507
@iddyramathan4507 2 жыл бұрын
Kumbe zanzibar ndio chimbuko la Tanganyika hatimaye Tanzania bila zanzibar Tanganyika Wala Tanzania hakika historia ya Zanzibar imekuwepo kabla ya ukoloni hivyo hakuna wa kuifuta Wala kupotosha historia yake kwani imetukuka Sana inaonyesha toka enzi hawakupenda Wala kuivumilia dhulma bali nguvu ya majeshi ya kikoloni.
@ahmedhamis
@ahmedhamis 20 күн бұрын
Tanganyika ilikuwepo miaka mingi sema Zanzibar kulikuwa na mwiingiliano wa watu wa mataifa
Always be more smart #shorts
00:32
Jin and Hattie
Рет қаралды 44 МЛН
Мы никогда не были так напуганы!
00:15
Аришнев
Рет қаралды 5 МЛН
КАРМАНЧИК 2 СЕЗОН 7 СЕРИЯ ФИНАЛ
21:37
Inter Production
Рет қаралды 493 М.
KUSIMAMA NA KUDONDOKA KWA DOLA YA ZANZIBAR #3
19:08
Bin Seif
Рет қаралды 31 М.
TAREIKH YETU MSIMU WA TATU (SILSILA 13): Shujaa Mkwawa, Sultani wa Wahehe
1:02:20
KUSIMAMA NA KUDONDOKA KWA DOLA YA ZANZIBAR #4
26:26
Bin Seif
Рет қаралды 37 М.
Телега - hahalivars
0:55
HAHALIVARS
Рет қаралды 2,5 МЛН
Love Challenge With Mellstroy And Mrbeast
0:19
BigSchool
Рет қаралды 7 МЛН
Don’t Bully a Vampire Girl 👿
0:38
Alan Chikin Chow
Рет қаралды 6 МЛН