Рет қаралды 14,037
Sayyid Said bin Sultan alizitawala Oman na Zanzibar kwa wakati mmoja baina ya miaka ya 1820 hadi kifo chake mwaka 1856. Alikichaguwa kisiwa cha Unguja kuwa makao makuu ya utawala wake na akalichaguwa eneo la Mtoni, kando kidogo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar, kuwa mahala pa kwanza kujenga nyumba yake iliyoitwa Beit Mtoni. Bwana Riadh Al Busaidi anaelezea ujenzi wa nyumba hiyo, uzuri wake na sababu za Sultan Said kuichaguwa Mtoni.