Рет қаралды 48,739
Waziri wa Maji Jumaa Aweso amewatia mbaroni Mhasibu na Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumiaji Maji wa kijiji cha Berege kilichopo Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma baada ya kubaini ubadhirifu wa fedha katika jumuiya hizo ambapo pia ameagiza kuvunjwa kwa Jumuiya hiyo na kutaka jumuiya zote nchini ziundwe upya kwa kuzingatia uwepo wa wataalamu wa maji na wahasibu wenye Taaluma.
Waliotiwa mbaroni na kupelekwa kuhojiwa katika kituo cha Polisi Wilaya ya Mpwapwa ni Scolastika Simbangulu, ambaye ni Mhasibu na Gideon Chesco Mwenyekiti wa Chombo cha watumiaji maji.
Aweso amesema jumuia hizo zimegeuzwa kichaka cha watu kugawana fedha hali inayozorotesha upatikanaji wa maji hivyo kila Jumuiya nchini zinapoundwa zizingatie uwepo wa watu wenye utaalamu ili kuepusha ubadhilifu wa fedha za maji.