Part8_Alichonijibu Mungu kuhusu ukweli wa Sabato|USHUHUDA WA RASHID NANJOTA ALIYEKUWA MUISLAM

  Рет қаралды 14,159

PROMOVER TV

PROMOVER TV

8 ай бұрын

Kutazama sehemu zilizopita bonyeza link hii • USHUHUDA WA RAYMOND/RA...
JE!UMEPENDA KAZI ZETU?BASI TUNAOMBA UCHANGIE SADAKA KILA MWEZI AU WAKATI WOWOTE ILI KUTUWEZESHA KUFANYA VIZURI ZAIDI.
M-pesa Lipa Namba.5634017
AirtelMoney Lipa No.3878783
Namba za mawasiliano/kuchangia sadaka ni: +255784074462 / +255766294335 / +254113844735 Majina ni Jacktan Msafiri
Kama uko tayari kuwa mchangiaji wa kila mwezi jiunge kwenye group letu la TEAM PROMOVER SUPPORTERS kwa kubonyeza link hii chat.whatsapp.com/CUGPFEt7SK4...
PIA UNAWEZA KUJIUNGA NA MAGROUP YETU MENGINE MAWILI AMBAYO PIA UTAPATA SHUHUDA ZETU MPYA KILA SIKU NA KUJIFUNZA NENO LA MUNGU
1.TZ PROMOVER TV USHUHUDA bonyeza link hii chat.whatsapp.com/J5QuMiNuG1l...
2.KENYA PROMOVER TV USHUHUDA bonyeza link hii chat.whatsapp.com/FRGK8R0u2ak...
#ShuhudaZaPromoverTv #Ushuhuda #PromoverTV

Пікірлер: 159
@PromovertvTz
@PromovertvTz 8 ай бұрын
Kutazama sehemu zilizopita bonyeza link hii kzbin.info/aero/PLXTmPgeqbJ0lf5zWXtk5KfQBHG7jJxnBn
@owenomwanawayesu6961
@owenomwanawayesu6961 8 ай бұрын
Mafunzo mema sana!
@JamuhuriIsaya
@JamuhuriIsaya 8 ай бұрын
​@@owenomwanawayesu6961Asante ndugu wengi tuna matatizo ktk hilo
@patrickkatana8823
@patrickkatana8823 8 ай бұрын
🇰🇪 I REALLY APPRECIATE YOUR TESTIMONY ..Najivunia Kristo kama Mwokozi wangu..🎉🎉
@josykogei7647
@josykogei7647 8 ай бұрын
Roho mtakatifu ni mwema, pia huelekeza mtu, Mimi nilisumbuka sana nikitaka kujua mbona Mungu anakubali watu wazidi kuwa wengi wakati anajua kunao wa kwenda jehanamu nilitamani kujua kwa mdaa mrefu ila mungu mwaminifu alinijibu yakwamba alihaidi ibrahimu uzao wake utakuwa kama mchanga wa bahari na neno lake halibatiliki kamwe nilfurai sana
@ester.k.6837
@ester.k.6837 8 ай бұрын
Je kuna wa-levites wa kuwapa zaka na sadaka zama hizi? Na kama tukichambua maandiko na kusema Haya ni kwa ajili ya wana wa Isreal tu, vipi kuhusu hizo amri 10 zingine? Vipi kuhusu zaka na sadaka? Ni kumuomba ROHO MTAKATIFU atufunulie binafsi!
@josykogei7647
@josykogei7647 8 ай бұрын
@@ester.k.6837 🤣🤣🤣 yesu is better to ask holy spirit my sister this mafarisayo watatupoteza God is faithful imgn ata ku direct
@eliaminkassembe463
@eliaminkassembe463 8 ай бұрын
Roho Mtakatifu huwaongoza watu kuelewa na kutii neno la Mungu. Roho anayeleta mtafaruku katika maandiko huyo ni roho mtakafujo na siyo huyo tuliyeahidiwa na Bwana Yesu kwamba yafaa mimi niondoke ili huyo roho Mtakatifu aweze kuja kwenu.
@emmymichaelchristopher4063
@emmymichaelchristopher4063 8 ай бұрын
Sisi sote tunaamini maandiko yote ktk biblia neno la mungu ikiwa linasema wewe unafunga wakati mungu kaisha kujulisha ndani biblia Inamaana wewe umini biblia. Yesu mwenyewe ndiye bwana wa sabato soma matayo 12;7,8 pia Luka 6: 4-6
@janetjanet8669
@janetjanet8669 8 ай бұрын
Na ubarikiwe sana mtumishi wa Mungu hata mimi nmefunguka macho yangu
@gracejaphet9985
@gracejaphet9985 8 ай бұрын
Amen mtumishi wa Mungu; nimebarikiwa sana na ufafanuzi wa sabato.Yesu Kristo ndiye Bwana wa Sabato.
@danpaulo8878
@danpaulo8878 8 ай бұрын
Nilikuwa nasubili kwa hamu sana mada hii,nashukuru sana mtumishi wa Mungu kwa majibu,nashukuru sana Promover TV kwa kutimiza ahadi ya kutuletea somo hili.
@samwelimwanja4105
@samwelimwanja4105 8 ай бұрын
Mtumishi uko sahihi 100% maana mimi mwenyewe hili suala lilinitatiza sana miaka ya nyuma ila baada ya kusoma vitabu mbalimbali vya watumishi wa Mungu nilipata kitabu kimoja Cha LYEKE UZORMA wa Nigeria nanukuu kile bwana Alichomwambia: kuhusu miaka, miezi, wiki, siku, na masaa yote hayo mbele za Mungu hayana maana. Akiwa na maana kuwa siku zote ni sawa mbele za Mungu na kumwabudu Mungu ni mda au Siku Yoyote. Ila upande wa kukutana ndio Binadamu amechagua iwe siku gani. Kwa hiyo Waabuduo j,pili na j,mosi wote ni sawa ila2 wakimwabudu katika Roho na kweli. Amen
@ellykibale190
@ellykibale190 8 ай бұрын
tunasemaje kuhusu amri ya nne (kutoka 20:8-11) ikumbuke siku ya sabato (siku ya Saba ya Juma ambayo ni jumamosi) ........ nisaidie kujua nini kimebadilika juu ya amri hii, katika agano letu jipya?
@annachachage4931
@annachachage4931 8 ай бұрын
​@@ellykibale190umejuaje kama hiyo siku ya sabato kama ni jumamosi?hiyo umeongeza wewe, imeandikwa ikumbuke siku ya sabato,ila haijaandikwa kama ni jumamosi, MUNGU alifanya kazi siku 6 siku ya 7alipumzika, lakini majina ya cku hayakuandikwa,fuatilia vizuri majibu ya mtumishi huyu yapo sahihi kabisa,
@maryandason1815
@maryandason1815 8 ай бұрын
​@@annachachage4931Amen❤
@samwelimwanja4105
@samwelimwanja4105 8 ай бұрын
@@ellykibale190 Hakuandika siku ndio maana siku zote ni sawa mbele zake ila kwa kuwa ametuumba tukiwa na Akili timamu basi tunaweza kuamua ni siku gani tukusanyikane pamoja ndio kama hiyo unayoiita wewe j,mos na mwingine j,pili
@ellykibale190
@ellykibale190 8 ай бұрын
@@samwelimwanja4105 Nilianza Kwa kupitia comment ili nipate idea/summary ya kilichojadiliwa , ila ngoja nipitie mahojiano, halafu nitarudi kuchangia
@user-lq6dd9pt7k
@user-lq6dd9pt7k 3 күн бұрын
Kaka,sasa wahubirie waislamu waache kupotea
@mwaminimwangaza
@mwaminimwangaza 8 ай бұрын
Amina tumwabudu siku zote kwasababu siku zote ni za Mungu, halleluya
@jesusfirstchurch4162
@jesusfirstchurch4162 8 ай бұрын
Kweli kabisa mtumishi siku zote ni za KUMWABUDU MUNGU maana siku zote ni za MUNGU 🎉
@johnzacharia
@johnzacharia 8 ай бұрын
Biblia. Wakolosai 2:16-17 [16]Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato
@AdventinaNdyanabo
@AdventinaNdyanabo 2 ай бұрын
Ubarikiwe kwa kunikumbusha ilo andiko
@sophiamakani6133
@sophiamakani6133 8 ай бұрын
Amen sanaa Mutumishi wa Mungu,Brother Jackson mwaja..mombasa kenya lini...Mungu awatangulie afanye njia.
@daudimichael7338
@daudimichael7338 8 ай бұрын
Yesu alikiri yeye ndiye Bwana wa Sabato, ndiye mwenye Sabato yake, aliponya siku ya Sabato, wanafunzi wake walipokuchua masuke siku ya Sabato, na hata mafarisayo walisema Yesu amevunja Sabato. Mafarisayo wapo mpaka leo (Wasabato), wasitutaabishe kama walivyotaka kumtaabisha Yesu wetu. 😂
@user-sf5gp5oi5k
@user-sf5gp5oi5k 7 ай бұрын
Asante Mungu maana na Mimi nilkua KWENYE mkanganyiko wa IPi siku sahihi Leo nmefunguliwa hakika Mungu ni mwema 🙏🙏
@pastorpetermageta6833
@pastorpetermageta6833 8 ай бұрын
Jactan Msafiri barikiwa kwa kuwaletea watumishi wa Mungu ujumbe kwa wakati mwafaka
@leahenockmrina5381
@leahenockmrina5381 8 ай бұрын
Mtumishi sasa amri za Mungu walipewa akina nani kama siyo waisrael kupitia Musa na sasa sisi je tunatakiwa kuzitii amri za Mungu ? Kama ni ndiyo mbona hiyo moja unaitoa kama ni hapana sasa sisi kanisa na sasa tunafuata amri ngapi? Hapa mtumishi bado naomba uzidi kuomba ili Mungu akujibu maana sisi wapentekoste tunang'ang'ania kuwa hakuna sabato lakini amri zingine tunazikubali kama Yesu Kristo amekuja na alisema Ndiye BWANA wa Sabato tukimwamini yeye tumeikubali sabato na kuitakasa na kuiheshimu Je mtumishi sisi Israel ya imani na ya siku za mwisho na kama wana wa Israel ni wana wa Ibrahimu kwa mwili na sisi tu wana wa Ibrahimu wa imani wa kanisa takatifu la siku ya mwisho sisi ni Israel ya imani uzao wa Ibrahimu kwa imani kwa hiyo kwa nini tupunguze amri zingine mtumishi naomba uchimbue zaidi maana wakristo wa kweli ni Israel ya imani na sabato tunatakiwa kuifuata nakuitakasa na kuifuata huku tukiamini katika roho mtakatifu na karama zake na matunda yake yote na kwa njia ya Yesu Kristo BWANA WETU.
@philipojangama
@philipojangama 8 ай бұрын
@@leahenockmrina5381 Mtumishi Hongera kwa kuendelea Kutafakari,Kwamimi nilivyomuelewa ni Kwamba Kuishika Sabato ni kustarehe,kupumzika,kuibariki na Kuitakasa kama Alivyofanya Mungu baada ya Kazi Siku 6,Sio swala la Kuabudu,Kuabudu ni Siku zote kama hiyo Jumamosi unabudu katika Roho na Kweli Mungu anapendezwa nawe,Watu wengi Mafundisho yao Sio kumpa Mungu ibada katika Roho na Kweli Bali Wanaipa Siku Heshima badala Ya Kumpa Heshima Mungu.Ubarikiwe!!!.
@gosbertmuta5421
@gosbertmuta5421 8 ай бұрын
Mbona nimempenda ghafla muonekano wake na ongeayake jamani hadi raha Mungu akutie nguvu asikupungukie kabsa
@user-cu3cl4yy5s
@user-cu3cl4yy5s 7 ай бұрын
Asante sanaaa mana hakika ni swali linanipaga shida sana na najiuliza kwanini hao waliokua wametekwa ktk ufalme wa shetani wakishuhudia hawajawahi kutaja kua makanisa ya kisabato yanampinga na kuharibu kazi za shetani
@user-cu3cl4yy5s
@user-cu3cl4yy5s 7 ай бұрын
Makanisa ya kilokole tuu ndio yametajwa kua ni ya kiroho na zinaharibu kazi za shetani na biblia inasema vita yetu c juu ya damu na nyama bali ni katika ulimwengu wa roho
@carolinemwugusi8945
@carolinemwugusi8945 8 ай бұрын
Mungu akubariki mtumishi wa Mungu kwa majibu haya mazuri na ya kuridhisha kupitia vifungu umeeleza vyema kabisa barikiwa pia promover tv kwa juhudi zenu kutufikishia ujumbe jinsi ipasavyo
@FatimahAlshehri-gt1gj
@FatimahAlshehri-gt1gj 8 ай бұрын
Amen mtumishi wa mungu umesema ukweli
@veronicamselle8103
@veronicamselle8103 8 ай бұрын
Amen, Mtumishi kamaliza utata. Nakuomba umtafute wa kuongelea kitimoto bwana mwamdishi @Jactani
@BENISiMBY
@BENISiMBY 16 күн бұрын
Hata Mimi nimesoma ya kwamba wanaohubiri sabato hawataingia mbinguni soma waebrania 4:4-5
@DoricEverist
@DoricEverist 8 ай бұрын
Mwenye sikio na asikie Mungu awajua waliowake ninaimani kunawatu ambao wamekusudiwa kupona kwenye huu ushuhuda Yesu anarudi na anataka kukusanya kondoo wake usishupaze shingo geuka sasa
@lydiamichael5509
@lydiamichael5509 8 ай бұрын
Zidi kuinuliwa mtumishi wa Mungu kwa somo hili
@user-rx2fi8eg6l
@user-rx2fi8eg6l 8 ай бұрын
Amen, YESU ndie Bwana wa sabato, Yoana 4:24 ndugu muema kutoka Kenya.
@queenesther8505
@queenesther8505 8 ай бұрын
Wakati wakristo wanafanya maombi ya katikati ya wiki,huwa kunatokea miujiza sana,haswa jumatatu hadi ijumaa,kiukweli mtumishi umesema ukweli kabisa,Mwenyezi Mungu aliumba siku hizi Zote.
@henryosoro7696
@henryosoro7696 8 ай бұрын
Mimi ni msabato,najazwa na Roho mtakatifu...hao wasabato wa huko walikujibu kimwili ,hawajui lolote.
@daudimichael7338
@daudimichael7338 8 ай бұрын
Basi wewe bila shaka siku ya kuabudu si shida kwako. Ubarikiwe.
@gosbertmuta5421
@gosbertmuta5421 8 ай бұрын
Asante 😅
@jacobmahona187
@jacobmahona187 8 ай бұрын
wa huko wapi tunawajua Sana wasabato NI Sheria tu na kukaririshwa maandiko Roho mtakatifu hakuna huko kwa wasabato!
@user-bx5nc8ge6r
@user-bx5nc8ge6r 8 ай бұрын
Ukiwa na roho mtakatifu na sabato utaijua sababu roho ndiye kiongozi
@esterpeter8556
@esterpeter8556 8 ай бұрын
Hakika Roho wa Mungu ni zaidi ya vyuo na elimu zote ,hata wasabato wenyewe awajawai kufafanua hivi , ubarikiwe Sana mtumishi wa Mungu
@oscarkalihamwe1621
@oscarkalihamwe1621 7 ай бұрын
Tushindwe kuona ufalme wa mungu tu kwa kuwa mioyo yetu inakibulii,, lakin ukweli tumeupata
@mariamfritsi4943
@mariamfritsi4943 8 ай бұрын
Asante sana kwa shuhuda.
@AzAz-sy6zp
@AzAz-sy6zp 8 ай бұрын
Amen ubarikiwe san mtumishi kwa ufafanuzi mzuri nimeelewa nashukuru
@lizhams8607
@lizhams8607 8 ай бұрын
Ukifuata Ushuhuda wa Domitira ule wa congo ameeleza kuhusu sabato , Yesu alimuabia yeye si wa dini.
@stephenlembo8986
@stephenlembo8986 8 ай бұрын
Mtumishi Jack ni vizuri sana mtu akipata neema ya kuokoka ahudhurie mafundisho ya wongofu wapya yana faida sana hasa wakipata waalim na wachungaji sahihi ,barikiweni sana.
@chrisdeoglatias8665
@chrisdeoglatias8665 8 ай бұрын
Sjamaliza kusikiliza ushuhuda had mwsho ila khs hili kwmb mtu ahudhurie Drs la waongofu wapy n zuri ila IJULIKANE KUWA km akaingia ktk madhabahu isiyoandaliwa na Yesu mwenyew ataishia tu kuwa shupavu WA kidini ila Bado uhtaji WA macho ya kiroho ndio mzr zaid. Maana ht watu WA DN wko hvyo huhudhuria kila mafunzo ya DINI Yao ila huishia kuyashika mambo ya DINI Yao tuu na sio fundsho la Mungu WA kweli. Kwhy hlo n zr lkn ikiwa atakuw ameangukia ktk madhabahu sahh vngnevyo afadhar afunuliwe na Roho Moja kw Moja maana huku kw Imani theology imetawala ht Roho Mt anakosea nafas y kuliingiza kanisa!
@dorcaskarago2876
@dorcaskarago2876 8 ай бұрын
Myaka michache iliyo pita Roho mtakatifu aliniambia ivo ivo
@RubenMtuwaMungu-bz8ee
@RubenMtuwaMungu-bz8ee 8 ай бұрын
Hao wasabato hawamjui Roho mtakatifu. Jambo ambalo ni muhimu zaidi ya sabato yenyewe
@danielmatemu9698
@danielmatemu9698 8 ай бұрын
Nakubaliana na wewe, wao wamebase zaidi kushika amri na maagizo hasa katika agano la kale. Lakini Roho Mtakatifu ndiye mwalimu wetu ambaue Kristo alituachia baada ya yeye kupaa mbinguni.
@user-mk6if8xs3s
@user-mk6if8xs3s 8 ай бұрын
Asante mtumishi kwa ufafanuzi huu Mungu akubariki ,Maana hata mch Petter Karim wa chamanzi alisema Mungu alimwambia siku zote nisbato ya Bwana, hakuna siku maalum ya kumwabudu yeye
@owenomwanawayesu6961
@owenomwanawayesu6961 8 ай бұрын
Mafunzo ya kweli kabisa!
@leahenockmrina5381
@leahenockmrina5381 8 ай бұрын
Mtumishi na lile neno alilosema Yesu Kristo kuwa hakuja kuitangua sabato bali alikuja kuitimiliza
@LoFi_120
@LoFi_120 8 ай бұрын
*sikuja kuitengua Torati bali kuitimiliza...
@PatrickMathias-cs9qc
@PatrickMathias-cs9qc 2 ай бұрын
Yesu hakusema sikuja kuitengua sabato alisema sikuja kuitengua torati bali kuitimiliza
@loisemuchiri8363
@loisemuchiri8363 8 ай бұрын
Nilikuwa na gonjea sana kuhusu hiyo swali
@Annsikoboy-ut8bs
@Annsikoboy-ut8bs 7 ай бұрын
Sabato ni agano la Mungu na Wanaisraeli. Nabii Musa aliwachukua waende kufanya Sabato wakati walikuwa Misri.
@piliechildofkingjesus4594
@piliechildofkingjesus4594 8 ай бұрын
Amen Amen Amen
@maryandason1815
@maryandason1815 8 ай бұрын
Amen blessed Kaka jacktan n Baba mtumish❤
@williammweta5539
@williammweta5539 8 ай бұрын
Amina mtumishi wa Bwana
@user-pg6kt6po3c
@user-pg6kt6po3c 8 ай бұрын
God bless you promovers
@samwelimwanja4105
@samwelimwanja4105 8 ай бұрын
Samweli from Singida Tz tupo Pamoja Promover tv.
@user-ek2oy8ot6q
@user-ek2oy8ot6q 8 ай бұрын
Amen
@samsonpopat1474
@samsonpopat1474 8 ай бұрын
Pole Sana kwa uwelewa huo roho wa Mungu hadhihakiwi na hakika atayatimiza mapenzi yake hata shetani mwenyewe alidiriki kumuambia Yesu imeandikwa huku akiyapotosha maandiko kidogo kwa uasi wake Yesu akamkemea na wewe pia si kosa lako ni kuchanganya mambo pole Sana Mungu akusaidie
@Richard0duori
@Richard0duori 7 ай бұрын
Kwa hivyo wewe unasemaje ?? Watu wa siku
@dastankalinga442
@dastankalinga442 7 күн бұрын
Wewe kama huamini 46:56 Roho mtakatifu hutajua maana ya sabato
@ebenezerchurchsupremetv9490
@ebenezerchurchsupremetv9490 8 ай бұрын
Hakuna mtu ambaye atapelekwa jehanamu kwaajili ya siku ya kuabudu,kama hujaokoka yaani kumpokea Yesu kristo
@JaneKyusa-xy9xz
@JaneKyusa-xy9xz 8 ай бұрын
Sabato ipo katika amri kumi za Mungu na ndio maana Yesu mwenyewe anasema ndie Bwana wa sabato kwa maana huwezi kumpenda Yesu halafu ukaikana sabato
@mwoso
@mwoso 8 ай бұрын
Ninakusihi ukutane au uwasiliane na mwalimu Ndacha mjadili kuhusu hili swala la sabato.
@dantez8775
@dantez8775 5 ай бұрын
Wasabato wanakanganya watu sana
@alexenderamon8009
@alexenderamon8009 5 ай бұрын
Hakika Biblia umesema kweli..,....Watu wengi wataangamia kwa kukosa maarifa(Ufahamu) hosea 4:6.....tusome Biblia wapendwa tusipotezwe na shuhuda za uongo
@fitinamarando
@fitinamarando 8 ай бұрын
Mtumishi endelea kueleza kwa ajili ya wale ambao hawakubahatika kusikia mwanzo
@alexenderamon8009
@alexenderamon8009 5 ай бұрын
Mzee ulianza vizuri sana ila kwa ufafanuzi wako juu ya sabato umekosea sana,umeniumiza sana maana umepotosha wengi sana daaah... Jamani tusome Biblia tutapata ukweli si kusikiliza tu..Bwana awabariki sana......Imesalia raha ya Sabato kwa watu wake..Ebrania 4:9.....Isaya 66:22-23 Hata mbingu mpya na inchi mpya zitakapofanywa wanadamu wote watapumzika na kumuabudu Bwana siku ya Sabato....
@patriciakalinga9176
@patriciakalinga9176 8 ай бұрын
Amen barikiwa
@EZRA-b1c
@EZRA-b1c 8 ай бұрын
AMEN AMEN ASANTE SANA
@nelsonkazaura5713
@nelsonkazaura5713 7 ай бұрын
Masikini Weee! Kweli Nimeamini Ya Kuwa Shetani Nae Hujifanya Kuwa Malaika Wa Nuru. Amekutoa ktk Giza Nene La Uislamu Akaja Kukumalizia Kabisa Kwa Kivuli Cha Ukristo! Tena Hizo Pumba Unadai Umepewa Na Roho Mtakatifu Kumbe Adui!
@NURU-YA-BWANA-TV
@NURU-YA-BWANA-TV 8 ай бұрын
Ameen Ameen
@user-xx6pz6ry8y
@user-xx6pz6ry8y 8 ай бұрын
Mwenye kuelewa ataelewa tu
@happnesskitumbo5713
@happnesskitumbo5713 8 ай бұрын
Exactly.
@user-ek2oy8ot6q
@user-ek2oy8ot6q 8 ай бұрын
Ukweli
@mwoso
@mwoso 8 ай бұрын
Hio siku ya mapumziko ya Mungu baada ya uumbaji, je ni amri gani alizo zitoa? Hasa kuhusu kuabudu? Tofautisha kati ya hio siku kuu ya Mungu na amri za Musa kwa Wana wa Israel.
@godisenzige7477
@godisenzige7477 8 ай бұрын
MUNGU ameiweka Sabato kuwa kama ishara kati yake na Wanadamu. Saa yaja na wote wamuabuduo Bwana watamuamudu katika Roho na Kweli. Ibada ya MUNGU inajengwa katika misingi miwili Roho (Roho Mtakatifu) na Kweli ( Mafundisho ya Mungu ) Siku zote tunapaswa kufanya Ibada maana ıbada ni sehemu ya kielelezo cha mahusiano yetu na MUNGU . lakini pia Agizo la MUNGU halipaswi kuachwa kwa ajili ya Busara za wanadamu. MUNGU anayetupenda sote anatujaza roho mtakatifu na kututumia popote tulipo kwa kadri apendavyo. Tuombe MUNGU Tutumike na baadae kukubalika kwake kwa kufuata MUONGOZO WA ROHO MTAKATIFU unaotuongoza kwenye KWELI yote. MUNGU awabariki wote . Neema ya BWANA itusaidie kujazwa Roho mtakatifu na kuenenda katika kweli yote.
@dastankalinga442
@dastankalinga442 7 күн бұрын
God
@JaneKyusa-xy9xz
@JaneKyusa-xy9xz 8 ай бұрын
Somen ufunuo 12:17 muangalie neno linasema nini ? halafu mtafakarii
@juliuskalama2746
@juliuskalama2746 8 ай бұрын
Nahakika huo ndio ukweli ambao nimekubaliana nao milele hata mimi nilisumbuka sana nanilipogundua, ukweli ukawa ndohuo
@fatumaminyeko1875
@fatumaminyeko1875 8 ай бұрын
Sikuzote nizakuabudu MUNGU, YESU akasema mwapotea kwamaana amjuwi madiko kisha akasema ikiwa puda wako amepotea siku ya sabato utakosa kumtafuta ?utamtafuta YESU die sabato
@eliaminkassembe463
@eliaminkassembe463 8 ай бұрын
Tusiwe wepesi kujifariji katika shuhuda za uongo za mtu. Biblia imesheheni ukweli usiopingika na kubadilishwa na mtu. Amri za Mungu ni za milele na Yesu anasema ukinipenda shika amri zangu. Huyu jamaa amekutana na shetani na kupewa ushuhuda huo, huyu amewapa faraja wengi wanaokataa kutii amri za Mungu. Huyu ni nabii wa uongo, na kwa sababu tumekaribia mwisho wa wakati, watu wengi wa namna hii watazuka na kuibuka. Nawasikitikia sana watu wengi ambao wamefurahi na kumwamini huyu jamaa. Ushauri wangu ni kuwa, tusomeni biblia kwa sababu humo ndiyo kuna ukweli wote badala ya kutegemea shuhuda za manabii wa uongo. Ndiyo maana kwenye uumbaji Mungu alimpatia akili kila mtu ili aweze kuelewa mapenzi yake.
@dastankalinga442
@dastankalinga442 7 күн бұрын
Yesu alitoa amri gani Yesu alisema amri mpya nawapa Pendaneni na hii ndiyo amri kuu
@loisemuchiri8363
@loisemuchiri8363 8 ай бұрын
Mimi lazima ni share na wasabato hapa Kenya juu hatupumui oooh hakika utauwawa siku ya kiama usioabudu siku ya saboto 😢 very confused
@carolinemwugusi8945
@carolinemwugusi8945 8 ай бұрын
Haki hatupumui
@maryandason1815
@maryandason1815 8 ай бұрын
Share kwa wote wasikiee
@jesuspower2390
@jesuspower2390 8 ай бұрын
😄 same here in Tanzania hatupumui hata... juu ya tusali on Saturday huh ..Sabatooo
@EsitaDavid2-wp1uf
@EsitaDavid2-wp1uf 8 ай бұрын
Usiwe na shida ,KUNA siku ya NANE watu walikuwa na kusanyiko makinu na KUTOA sadaka.suku ZOTE tuwe Katia Roho na kweli.
@miltonjohn9779
@miltonjohn9779 5 ай бұрын
Easabato na waislam hawana utofauti
@JaneKyusa-xy9xz
@JaneKyusa-xy9xz 8 ай бұрын
Sabato ifanyika kwa ajili ya mwanadam
@bettymartha2306
@bettymartha2306 8 ай бұрын
Isaiah 66:22:24 Hapa bibilia ina sema wanadamu wooooote including you and me sio waisraeli pekee,,,,,,ni wote watakao ingia ule mji Jerusalem mpya na sabato itakua,,,,,,,,,, Mutimishi soma bibilia vizuri na uelewe.
@andrewkissava9184
@andrewkissava9184 8 ай бұрын
We bettymartha wewe ni msabato mbishi hivyo huwezi kuelewe hebu sikiliza halafu chukua hatua
@bettymartha2306
@bettymartha2306 8 ай бұрын
@@andrewkissava9184 Mimi nitaelewa bibilia pekee sio mwanadam and the bible can not contradict it self,,,, Amen? Sabato sio ya waisraeli Bali ya wanadamu wote...and thatz why yesu ni bwana wa sabato ndugu.
@sarahkishaluli6087
@sarahkishaluli6087 8 ай бұрын
Wakolisai 2:16
@user-bx5nc8ge6r
@user-bx5nc8ge6r 8 ай бұрын
🤔yesu fanya urudi
@EZRA-b1c
@EZRA-b1c 8 ай бұрын
Mimi natamani Yesu Arudi lakini inauma.sana.wengi bado ni vipofu na.viziwi na wakaidi hawataki KWELI ili wawekwe.HURU. Kipindi cha Nuhu na Kipindi cha Lutu ilikuwa hivi hivi! Let's watch out wana wa Mungu
@AW-vt9pw
@AW-vt9pw 8 ай бұрын
Hapo naona mnalumbana wenyewe kwa wenyewe Yaani wakiristo.
@user-dy2id4mz3k
@user-dy2id4mz3k 8 ай бұрын
Mapambo je mtumishi
@maryandason1815
@maryandason1815 8 ай бұрын
We uko wp mapambo yote n dhaMbi , jehanam unaenda bila ubishi
@CherieDeDieu
@CherieDeDieu 8 ай бұрын
Angalia mafunzo za Mchungaji Amieli Katekela hapa hapa Promover. Amezungumzia mara kadhaa.
@samjosh12
@samjosh12 8 ай бұрын
Andaa kipindi kabisa ili atililike
@-TECHNICIAN
@-TECHNICIAN 8 ай бұрын
JE KWA SASA AMESHALUDIANA NA YULE MKE WA PILI ULIYE FUNGANAYE NDOA HAPA DAR BAADA YA MKE WAKE WA KWANZA KUFARIKI UKO SINGLE MTUMISHI ...??
@FatimahAlshehri-gt1gj
@FatimahAlshehri-gt1gj 8 ай бұрын
Pia mmi nilitaka kujua ilo swahili
@joshuabartonpolelaab4985
@joshuabartonpolelaab4985 8 ай бұрын
yuko single@@FatimahAlshehri-gt1gj
@bonniebaraka
@bonniebaraka 8 ай бұрын
Ukimaliza kuhusu sabato tuambie kuhusu mama ellen white na maono yake 1844
@josykogei7647
@josykogei7647 8 ай бұрын
Hiii nikujichunga na chachu ya mafarisayo
@gosbertmuta5421
@gosbertmuta5421 8 ай бұрын
Nyie huyu ni Paulo wapili ase amejawa na hekima ya ajabu
@annachachage4931
@annachachage4931 8 ай бұрын
Je sheria ya kutoa zaka au fungu la kumi imekaaje,wakristo tunafitilia sana hii tu lakini kulikua na matoleo mengi sana je tunapofuata hii moja tu,nakuacha matoleo mengine inakuaje hii ilikua inatuhusu sisi kweli? maana ukikosa juu ya amri moja umekosa zote?naomba nisaidiwe Malaki 3:8-10,inatuhusu kweli?
@BENISiMBY
@BENISiMBY 16 күн бұрын
Hata fungu la kumi halifai kutolewa kwa sasa soma wagalatia 1:6-9 kwa sababu Yesu na mitume hawakufundisha ebrania 8:13
@Cairomari
@Cairomari 8 ай бұрын
Lakini si sisi tumefanyika wana wa Israeli kwa damu ya dhamana ya Kristo mtumish?
@rerisamba
@rerisamba 8 ай бұрын
Mimi nionavyo hili swala la sabato niligumu heri likabaki vile lilivyo tu coz ukisema ati agano lilikua nila taifa la Israel sioni kama ni sawa coz kuna hixo amri zingine 9 je sitakua ni za taifa la Israel
@RubenMtuwaMungu-bz8ee
@RubenMtuwaMungu-bz8ee 8 ай бұрын
Ellen G White ni nabii wa uongo hamtambui Roho mtakatifu Wala nafsi tatu za Mungu.
@leahenockmrina5381
@leahenockmrina5381 8 ай бұрын
Hata mimi simuelewi kusema lilikuwa ni la Israel wakati wakristo nao ni Israel ya imani
@watotowetutv9152
@watotowetutv9152 8 ай бұрын
​@@RubenMtuwaMungu-bz8eeunaushahidi?
@watotowetutv9152
@watotowetutv9152 8 ай бұрын
​@@RubenMtuwaMungu-bz8eeunaushahidi?
@annachachage4931
@annachachage4931 8 ай бұрын
YESU alipokuja alileta amri mpya yohana 13:34 pia warumi 13:9 ukishika hayo mpendwa ufalme unaishi ndani yako daily,
@juliuskalama2746
@juliuskalama2746 8 ай бұрын
Nimekubaliana na wewe kabsa
@stellaelias8174
@stellaelias8174 8 ай бұрын
Wasabato ni mafalisayo soma yohana 9.1-41
@eliomondioloo
@eliomondioloo 8 ай бұрын
Sabbath was given to Adam in the garden of Eden and was written by God fingers on tablet of stones twice remember Moses broke the first and God told him to prepare two set of stones and God wrote again. since Jesus is the same,today and forever Heb13:8.I doubt this brother revelation for Almighty God cannot remove one Commandment from what He wrote and keep the rest 9 but do away with this And if you argue Jesus fulfilled them then Catholic are correct in removing also the second commandment to make images of Jesus and worship them
@hillarymecha2839
@hillarymecha2839 8 ай бұрын
Colossians 2:16
@badruseif1318
@badruseif1318 8 ай бұрын
Babu ana PHD ya uwongo uyo
@daudimichael7338
@daudimichael7338 8 ай бұрын
Tupe PHD yako ya ukweli😂
@valentinanduku8718
@valentinanduku8718 8 ай бұрын
Tupee yako ya ukweli
@asbornkaduga6001
@asbornkaduga6001 8 ай бұрын
Kuna wasiwasi hapo kwenye Roho mtakatifu na Amri kumi za MUNGU mbona kama mfananiaho huo auendani , Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 2 Wakorintho 11:14 Shetani mwenyewe anayajua maandiko ndio maana umeitambua Sabato kwa uelewa wako, Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 2 Petro 3:9
@raymondnanjota5934
@raymondnanjota5934 8 ай бұрын
Jambo muhimu ambalo watu wa Mungu mnatakiwa kufahamu ni hili. Agano ni kuu kuliko amri,sheria,na maagizo. amri ya sabato na amri zingine zote walizo pewa wana wa Israel, ni kipengele tu katika agano la kale. au agano alilolifanya Mungu na wana wa Israeli. Agano linakamilika kwa kukusanya vitu vyote, ikiwemo amri kumi za Mungu, kopo la mana, fimbo ya Haruni. Vyote hivyo vilifungwa katika sanduku moja la agano. Hilo ndilo agano lenyewe, amri kumi tu hazikamilishi agano la Mungu kwa wana wa Israeli. Pasipo damu ya agano, agano la Mungu haliwezi kuthibitika. Musa alitwaa damu katika bakuli akanyunyizia madhabahu, ndipo akitwaa kitabu cha agano akakisoma, akatwaa damu akawanyunyizia wale watu na kuwaambia hii ndiyo damu ya agano. Kutoka 24:6-8 Agano jipya pia, lilifanywa na Yesu na wanafunzi wake kwa ajili ya ondoleo la dhambi kwa ulimwengu wote. Nalo agano jipya halikufanyika pasipo damu. Damu ya agano jipya siyo damu ya mbuzi,kondoo na ng'ombe bali damu ya Yesu kristo. Mathayo 26:26-28. Kwa kuwa maagano mawili hayawezi kufanyakazi katika kizazi kimoja, au hayawezi kusimama katika msingi mmoja. Lazima moja litoweke moja kibali. Ebra 8:7,13 Ebra 10:9-10 Kwakuwa mambo yote yanayo nena torati unena juu ya hao walio chini ya torati. 3:33 Wanaokombolewa katika agano jipya mambo yote ya ukombozi yamekamilishwa katika Roho mtakatifu. 2petro 1:3-4 Lakini kama mtu amechagua kuongozwa na amri kumi za Mungu, maanayake amechagua kukombolewa kwa damu ya mbuzi na kondoo. Lakini mimi nimechagua agano jipya ili nikombolewe kwa damu ya Yesu kristo, kisha nitiwe muhuri wa Roho mtakatifu. Tatizo kuu linalo wafanya watu wengi wa Mungu wasiiamini injili ya Yesu kristo, Kila wanapoisoma torati ya Musa utaji uleule uliowakalia wana wa Israeli na washika amri nao huwakakia. Wasizukiwe na nuru ya injili ya Kristo. 2kor 3:13-18 Nina mengi kuhusu sabato na amri kumi za Mungu, ambayo Roho wa Mungu amenifundisha Mungu akitupa uzima utaandaa semina mwaka huu, tuta iweka hewani promover tv. Mungu awabariki nyote nakaribisha maswali yenu.
@user-jt9ny6lg6v
@user-jt9ny6lg6v 8 ай бұрын
Hakuna jmapili kwenye biblia ila sabato tu tunaona hata uumbaji alimaliza siku ya ijumaa hakuna sabato ya kufanya kazi wakati tumepewa siku sita
@mcchilo13
@mcchilo13 7 ай бұрын
Acha kuongeza maneno yako mwenyewe. Biblia haijataja Siku pale. Hakuna jumatatu wala jumamosi pale.
@mcchilo13
@mcchilo13 7 ай бұрын
Kwanza ukihesababu kuanzia jumamosi. Maana ya jumamosi ni juma la kwanza. Ukihesabu Siku ya saba inaangukia ijumaa. 😮😮
@user-ek2oy8ot6q
@user-ek2oy8ot6q 8 ай бұрын
Amen
@user-xx6pz6ry8y
@user-xx6pz6ry8y 8 ай бұрын
Mwenye kuelewa ataelewa tu
@RubenMtuwaMungu-bz8ee
@RubenMtuwaMungu-bz8ee 8 ай бұрын
Hao wasabato hawamjui Roho mtakatifu. Jambo ambalo ni muhimu zaidi ya sabato yenyewe
@sophiamakani6133
@sophiamakani6133 8 ай бұрын
Share kote kote
@maryandason1815
@maryandason1815 8 ай бұрын
Tena wabish saana usiombe kukutana n wasabato washika din Cha ajabu Roho Mt.awamtaki😢Sasa cjui wakikutana wote kuabudu wanamwabudu nan😢
@user-xx6pz6ry8y
@user-xx6pz6ry8y 8 ай бұрын
Mwenye kuelewa ataelewa tu
@josephmutemi7494
@josephmutemi7494 8 ай бұрын
Amen
@user-xx6pz6ry8y
@user-xx6pz6ry8y 8 ай бұрын
Mwenye kuelewa ataelewa tu
Vivaan  Tanya once again pranked Papa 🤣😇🤣
00:10
seema lamba
Рет қаралды 33 МЛН
I Can't Believe We Did This...
00:38
Stokes Twins
Рет қаралды 90 МЛН
HOW DID HE WIN? 😱
00:33
Topper Guild
Рет қаралды 40 МЛН
JINSI YA KUPONA MAUMIVU ULIYOPITIA - JOEL NANAUKA
6:40
Joel Nanauka
Рет қаралды 31 М.
USHUHUDA WA KILICHO MFANYA OSINACH KUTOKUINGIA MBINGUNI
23:22
SHUHUDA ZA KWELI
Рет қаралды 42 М.